Friday, June 5, 2020

MWANAUME AKIKUAMBIA HIVI JE NI DHARAU AU NI UPENDO?

Tags


Najua ushajiuliza swali hili, kama mpenzi wako kakuomba hicho kitu unajiuliza je hivi ni kwamba ananipenda sana ndiyo maana anataka nimpe kila kitu ili asichepuke au ananidharau sana kaniona Malaya ndiyo maana kaniomba. Jibu nikuwa ni dharau sana, kama mwanaume kafikia hatua ya kukuomba hivyo basi jua kakudharau mpaka mshipa wa mwisho.
Mara nyingi wanaume huwaomba huo mchezo Malaya au wanawake ambao hawana ampango nao. Kwamba anataka kukuacha lakini haoni sababu hivyo anakuomba ukikubali poa ukikataa poa. Ukikubali anaendelea na wewe hakuachi mpaka pale atakapopata mwanamke wa heshima wa kuoa ndipo hukucha au anakuoa lakini akikuchoka basi hukuacha kama wale wengine tu!
Mwisho nimalizie kwa kusema, najua unaamini kuwa anakupenda, najua unaogopa kua atakucha lakini kama hicho ndiyo kigezo alichokupa ili akuoe Dada yangu muambie aondoke tu kwani hata akikuoa atakuja kukacha tu au kukutelekeza. Iko hivi mwanaume ambaye hufanya huu upuuzi na mkewe basi kuna mawiali, kwanza inawezekana kashamchoka muda mrefu na anamtafutia sababu ya kumuacha lakini pili nikuwa kashakua addicted mpaka basi.
Kwamba hawezi kujizuia tena na anakuja kukuambia kwakua huko nnje mabinti wote anaotembea nao ashawaharibu anaona akuharibu na wewe na akimaliza nahamia kwingine. Sasa kama una akili ushanielewa lakini kama bado unawaza ndoa usijali endelea kufanya, wewe mpe tu na siku ukianza kuvaa nepi hata mimi mtu akiniomba ushauri nitamuamba acha ujinga muache.
Kwani kama unakubali kufanya hivyo sidhani kama unafaa hata kuwa mke wa mtu! Siwezi kumshauri mwanaume mwenzangu kubeba mzigo ambao atalia nao maisha yake yote maana najua ni miaka miwili tu atakua ashakuchoka. Sana sana akiniomba ushauri nitamuambia aache atafute msaada wa kitaalamu na aende kuoa mwanamke anayejigheshimu mpya kabisa asifanye tena huo upuuzi!
Najua una rafiki yako ambaye anafanya, anakuambia haina shida hivyo wala usiogope. Kama yuko anakuambia hivyo basi jua anatafuta mwenzake wa kusema mbona naflani naye anafanya lakini pia jua kuwa akianza kuvaa nepi hatakuambia kwani hiyo ni aibu ambayo kila mtu hubeba kivyake. Lakini jua mume akishakuona unavaa nepi hutamuona tena ataenda zake kutafuta vibinti vipya kabisa wewe utaishia kusema “Namuachia Mungu!”



EmoticonEmoticon